Ads 468x60px

SOCIAL FLOATING

Get this

Sunday 6 January 2013

HUU NDO UHASAMA NA CHUKI BINAFSI ZA WASANII WETU

TID vs Ali Kiba Beef hii ilianza baada ya Ali Kiba na familia yake kumshutumu TID kuwa alikuwa amepanga njama za kumuua Ali Kiba. Tuhuma hizo zilipelekea TID kupelekwa polisi lakini alitoka baada ya kesi hiyo kuonekana haina ushahidi wa kutosha. Mpaka sasa TID bado ana hasira na Ali Kiba na hivi karibuni kupitia Facebook alimuita ‘homo’ kutokana na kitendo chake cha kumtupia shutuma hizo. “Stupid Thing Ever Happened in Bongo Music Scene is this Homo mentioned me Trying to Kill Him while am only thinkin about this Girl…No Homo,let’s make Hits,” aliandika TID. AY vs Hermy B
Uhusiano kati ya Hermy B na AY waliokuwa maswahiba wa muda mrefu uliingia dosari baada ya kile kinachodaiwa kushindwa kuelewana katika bei mpya ya kurekodia wimbo katika studio za B’Hits. Hermy B aliwataka AY na MwanaFA kulipia kiwango kikubwa zaidi kwa single wanazorekodi kwakuwa wao ni wasanii wakubwa kitu ambacho hawakukikubali na kuamua kuvunja uhusiano na B’Hits. Baadaye Hermy B alikuja kuandika barua mbili tofauti kuelezea jambo hilo na jinsi uhusiano wao ulivyovunjika. AY alidai angekuja kuandika maelezo kwa upande wake lakini hata hivyo hakuandika. Miongoni mwa aliyoandika Hermy kwenye barua ya kwanza ni: Kilichotokea ni kwamba, mwaka huu mwanzoni kabisa, A.Y aliwasiliana na mimi akiwa na mipango ya kuzindua albamu yake. Na alitaka kuzinunua zile nyimbo kutoka kwangu akiwa na mpango mpya wa kuiuza albamu kwa mpango wake binafsi pasi na mimi. Nilishindwa kuelewa nini anakifanya hasa alipoomba alipie wimbo mmoja mmoja tena kwa bei ya msanii wa kawaida anaehangaika kutoka. Niliamua kukubali kwamba ameamua kufanya hivyo na sina nguvu ya kumzuia basi nikajaribu kupata malipo halisi ya kazi yangu. Ubishi wangu ulikua kwamba msanii mdogo hawezi kulipa bei sawa ya kurekodi na msanii mkubwa, kwani hata malipo ya msanii mkubwa na mdogo baada ya kazi yoyote iwe ya matangazo ama show huwa hayafanani. Bei niliyotaja haikua millioni kumi, ni uongo mtupu na kwa wimbo mmoja niliomba nilipwe millioni 2. Akakubali kwa bei hiyo ya Millioni 2 japo nilihisi hakuridhika kabisa. Nilimtumia mkataba wa makubaliano yetu ambayo kweli baadae aliona kwamba bei hiyo kwake ni kubwa sana hivyo hatukusaini makubaliano. Tulibadilishana meseji kwa simu kwa muda mrefu sana na niliona biashara hii itavunja urafiki wetu. Nilifikiria sana kwamba nyimbo hizi nimekaa nazo toka 2008 bila kuingiza chochote na maisha yanaenda pia. Sikuona sababu ya kuharibu urafiki wetu wa muda mrefu kwa mabishano haya. Kwa Ujumbe wa simu nilimueleza A.Y anakaribishwa aje achukue nyimbo zoooooote anazohitaji kwa albamu yake BURE (bila malipo).Lakini nilimuomba anisamehe sitomix zile ambazo bado hazijamixiwa, ila ampatie producer mwingine amfanyie hiyo kazi. Mpaka naona hii makala A.Y hajaja kuchukua hizo nyimbo na ndio naelewa kua hayupo na BHits tena na wala taarifa zote hizo mbili hajawahi kunipatia. Huu ndio ukweli halisi. Lord Eyez vs Ommy Dimpoz
Beef hii ilianza baada ya Ommy Dimpoz kupost picha za Lord Eyez kwenye mtandao wa Twitter akiwa amekamatwa kwa kile alichodai kumuibia vifaa vya gari yake. Picha hizo zilisambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii na websites/blogs. Baadhi ya watu walimlaumu Ommy kwa kitendo hicho cha kumwanika mwanamuziki mwenzie. Baada ya kukamatwa na polisi na baadaye kutoka nje kwa dhamana wakati kesi hiyo ikiendelea, Lord Eyez alirekodi wimbo Bongo Records ambamo anasikika akimtaja Ommy Dimpoz.

No comments:

Post a Comment

 
Powered By Blogger

Sample Text

life is all about showing people what you gat

Translate